2024-08-21 05:00
Mithali 7:1-5
1 Mwanangu, yashike maneno yangu, Na kuziweka amri zangu akiba kwako.
2 Uzishike amri zangu ukaishi, Na sheria yangu kama mboni ya jicho lako.
3 Zifunge katika vidole vyako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
4 Mwambie hekima, Wewe ndiwe umbu langu; Mwite ufahamu jamaa yako mwanamke.
5 Wapate kukulinda na malaya, Na mgeni akubembelezaye kwa maneno yake.
Neno la Bwana!